1 Corinthians 10:1-5

Onyo Kutoka Historia Ya Waisraeli

1 aNdugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari. 2 bWote wakabatizwa kuwa wa Musa ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari. 3 cWote walikula chakula kile kile cha roho, 4 dna wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Al-Masihi. 5 eLakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.

Copyright information for SwhKC